Home » » Vita Kawawa aishauri serikali

Vita Kawawa aishauri serikali


JIBU LA SWALI LA MBUNGE Namtumbo

SERIKALI imetakiwa kutoa kazi kwa makandarasi ambao wameonyesha uwezo katika kutekeleza kazi zao na kukamilisha miradi ya ujenzi wa barabara  ya kutoka Songea –Mbinga na kutoka Mbinga – Songea kwa wakati na kuachana na makandarasi wababaishaji ambao wamekuwa wakiisumbua serikali.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni mjini hapa na Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa (CCM), wakati alipokuwa akiuliza swali la msingi.
Katika swali la msingi mbunge huyo alitaka kujua ni lini mkandarasi mwingine atapatikana ili kazi ya ujenzi wa barabara hiyo uweze kukamilika kama ilivyokusudiwa.
“Serikali ilimsimamisha mkandarasi wa barabara ya Namtumbo-Tunduru kutokana na kutofanya kazi yake inavyotakiwa kwa mujibu wa mkataba,” alisema mbunge huyo.
Akijibu maswali hayo kwa pamoja Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Gerson Lwenge, amekiri mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Namtumbo-Tunduru kuwa ilifika mahali akaonekana ni mbabaishaji, hivyo kusimamishwa.
Aidha, alitoa wito kwa makandarasi ambao wana uwezo kujitokeza na kuomba tenda mara tu zinapotangazwa ili waweze kupewa kazi hizo kwa kuwa tayari kazi yao ya awali itakuwa imeonekana.
Naibu waziri huyo alisema suala la kuomba tenda ni utaratibu ambao upo na unatakiwa kufuatwa na makandarasi wote. Alisema mchakato wa kuwapata makandarasi wengine kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya Namtumbo –Tunduru kwa kiwango cha lami unaendelea.
Alifafanua kuwa tenda ya ujenzi wa barabara hiyo ilitangazwa Septemba 1, 2013, na kuongeza kuwa wazabuni walitembelea barabara hiyo Septemba 19, 2013 ili waweze kujaza zabuni zao.
Lwenge alieleza kuwa zabuni hizo zilifungwa Novemba 12, 2013 ili kazi ya kutathmini ianze, lengo likiwa ni kuwapata makandarasi mapema iwezekanavyo.

chanzo;tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa