Home » » MAFUNZO YA VIJANA WA CCM YAFUNGWA MKOANI RUVUMA

MAFUNZO YA VIJANA WA CCM YAFUNGWA MKOANI RUVUMA

 Kwa ukakamavu kijana wa CCM akimvisha kitambaa Mh.Mwigulu nchemba mara baada ya kuwasili kwenye kambi ya mafunzo ya vijana wa CCM-Namtumbo
 CCM oyeeeeee!!!Naibu katibu mkuu akisalimiana na vijana wa CCM wakati akiingia eneo la tukio.
Naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania bara ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi Mh.Mwigulu Lameck Nchemba leo Tar.31/10/2013 amefunga rasmi mafunzo ya vijana wa CCM (UVCCM) yaliyofanyika kwa muda wa wiki mbili hapa Ruvuma Wilaya ya Namtumbo.Mafunzo haya yaliyojumuisha wilaya zote za Ruvuma kwa vijana wa CCM yalilenga kuwajengea uwezo vijana wa kutambua Umuhimu wao katika kushiriki kwenye shughuli za maendeleo ndani ya nchi yao,siasa za nchi na mwenendo wake,Uelewa kuhusu namna ya kufanya maamuzi sahihi katika umri wake huu wa ujana,pia kuwaandaa kifikra na kimaadili kwaajili ya kuijenga na kuimarisha CCM pamoja na jumuia zake hasa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi.
 
 Vijana wakiwa na nyuso za Furaha baada ya kuonana uso kwa uso na Kiongozi wao wa chama wa ngazi ya taifa.Mh.Mwigulu nchemba
Akizungumza kwa mifano mingi iliyohai ndani na nje ya nchi yetu,Mh.Mwigulu Nchemba wakati wa kufunga mafunzo ya vijana wa CCM amezungumza na vijana wote waliokuwepo kambini(Vijana 450) na kuwasihi sana kuwa makini na mambo makuu matatu,Moja ni kuhusiana na Uandishi wa katiba mpya,Pili amezungumzia kuhusu rasilimali za nchi na mwisho amesisitiza kuhusu Umuhimu wa vijana kujitambua hasa ukizingatia Taifa letu linapita katika kipindi aambacho vijana ni wengi sana kuliko rika lolote lile.
 
 Hapo vipiiii???ni ishara ya dole(mambo sawa) kutoka kwa Naibu katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi.
Akianza kwa kuzungumzia Mchakato wa uandishi wa katiba Mpya,Mwigulu Nchemba amewaomba vijana kuwa makini sana na propaganda zozote zile wanazozisikia kutoka kwa watu wengine kuhusu kufanya vurugu ili katiba isipatikane.Amesema mchakato wa katiba umekwenda vizuri na umezingatika matakwa ya kila kundi na Taasisi licha ya Taasisi zingine kutaka maoni yao yawe bora kuliko ya watu wengine,"Katiba hii si ya CCM na sio ya chama chochote kile au mtu yeyote yule ni katiba ya Watanzania wote bila kuangalia rangi,kabila,chama,maumbile ya mtu n.k .Maoni yamekusanywa na kufanyiwa tathimini na tume husika na sasa tunaelekea hatua za mwisho za kupata katiba mpya.Hivyo basi nawaomba sana vijana wa CCM na vijana wengine wote kuacha kujiingiza kwenye makundi na mkumbo wa kugomea mchakato wa katiba mpya,kwa sababu hao wanaowahimiza kugoma wao wenyewe wanaajenda yao ya siri kuhusu Taifa hili.Ni kawaida yao kugoma,ni kawaida yao kupinga kila kitu,Kila mmpja wetu alipewa nafasi ya kutoa maoni kupitia taasisi na wanachama wake,Kuna wenzetu walikuwa wanafanya mikutano ya hadhara,hii yote ni kuhadaa na kudanganya watanzania."alisema.
 
Namshukuru sana Rais kikwete kwa kuwapa somo wapinzani kwamba maandamano si suruhisho na jambo lolote zaidi ya kudumaza maendeleo,Yawezekana walikuwa natafuta sehemu ya kula ruzuku za vyama vyao sijui!!Lakini tujiulize ni mapenzi gani haya ya jioni?Ni ndoa gani hii ya watu watatu ya usiku?Wapi na wapi hawa watu wakaungana eti kutetea maslahi ya Watanzania.?.
Hivyo nawaomba sana vijana muache kabisa kabisa kujihususisha na uvunjifu wa amani au kugomea jambo lolote la kitaifa.Kama linakwenda vibaya vyombo vya kusemea vipo na serikali inawapa nafasi hiyo.
Jambo kuwa nawahakikishieni vijana wa CCM,Kwa namna CCM tulivyoimara iwe kwa katiba ya sasa au mpya au katiba yoyote CCM tutashinda kwa sababu tunajiamini,tunakubalika kwa watanzania,tunamtandao mkubwa sana na jumuia yetu moja tu kama hii ya vijana ni kubwa kuliko CHADEMA yote na vyama vingine.

 Vijana wakifurahia jambo kutoka kwa mgeni rasmi Mh.Mwigulu Nchemba
Jambo la pili Mh.mwigulu Nchemba amezungumzia kuhusu rasilimali za nchi na namna vijana wanatakiwa watumie fursa husika kuzilinda mali na kujitengenezea mazingira ya ajira kwa siku za karibuni.Mwigulu amewasisitizia vijana kuwa serikali imejenga barabara kutoka Dsm hadi Namtumbo kwa kiwango cha rami na barabara hiyo imeunganishwa mikoa yote ya Tanzania.Hivyo rasilimali za nchi ni lazima zilindwe ilikunufaisha wazawa/watanzania wote na sio watu wachache.Ameomba vijana kulinda rasilimali za nchi yao na kauchana na wajasiliamali wa mataifa makubwa ambao wamekosa uzalendo ndani ya nchi yetu na wanaingia mikataba ya vyama vya nje ya kuwapa masharti eti wakichukua dola watagawana rasilimali zilizopo.
 
 Naibu katibu mkuu akitoa kadi ya uanachama wa UVCCM kwa mmoja wa vijana wa CCM waliohudhuria mafunzo hapa Namtumbo.
Swala la ulinzi na usalam wa Taifa letu ni la kila mmoja wetu vijana,hakuna kuwapa nafasis watu wasio litakia mema taifa letu.Serikali ya CCM imejipanga kuhakikisha rasilimali zilizopo zinanufaisha wananchi wote.zinalindwa kwa namna yoyote ile.Nimesikia kuwa kuna wasiasa wanakuja kuwaomba mfanye maandamano na vurugu kuhusu mali za nchi yenu,Wapuuzieni hao kwasababu nyie wenyewe mnaona kazi zinazofanyika na serikali yenu na namna rasilimali zinavyotumika kwa manufaa yoyote.Hapa Namtumbo na mkoa mzima wa Ruvuma miradi ya serikali ya mingi imeshatekelezwa ya barabara,Umeme na afya ambayo ni kazi ya serikali ya CCM kupitia kodi na manufaa ya rasilimali zetu.Naomba sana mtumie ujana wenu kulinda mali za nchi na kuipigania CCM iendelee kuongoza nchi yetu kwa miaka mingi zaidi kwa sababu nje ya CCM vyama vingine ni wababishaji tu na wanajenda zao na ndugu zao huko kwenye mataifa ya nje.
 Mh.Mwigulu Nchemba akizungumziza na mamia ya vijana wa CCM wakati wa kufunga mafunzo.
Msiwe kama watu wa Misri ambao hadi leo hawalewi wanachokihitaji,kwa sababu walimuondoa Rais wao wa aliyekuwepo madarakani,wakamuweka wakwao,ndani ya miezi sita wamemng'oa waliomuweka wanasema bora yule wa kwanza.Leo hii ukiwauliza wanataka nini watakwambia hata hawajui wanataka nini.Nchi yao imeshagawanyika na amani hairudi tena kirahisi.

Tatu,Naibu katibu Mkuu ametoa somo kwa vijana wa CCM namna ya kuendana na hali halisi ya Taifa letu hasa idadi kubwa ya vijana kuliko rika lolote ndani ya nchi.Vijana ni wengi sana na wengi hawana ajira za kutosheleza mahitaji yao.Hivyo wingi wa vijana,Mh.Mwigulu anasema ni lazima vijana watumia muda na akili zao vizuri ilikuepukana na makundi hatarishi ya tabia na maisha yao,kujiepusha na vyama vinavyohangaika huku na kule kuhakikisha nchi yetu haitawaliki.
 Zaidi ya vijana wa CCM 450 waliokaa kambi wiki mbili kujifunza namna ya kuongoza,siasa na utendaji wakimsikiliza Mh.Mwigulu Nchemba.
Nanukuu"Nimekuwa kijana kama nyie,nimepitia umoja wa vijana wa chama changu cha CCM,Nilijituma kujihusisha na kazi za maendeleo ya chama na nchi yangu,Niliepukana na makundi yasio na tija kwangu na nilitii kile wakubwa walichonielekeza ndio maana leo nimefikia katika hatua kubwa kama hii ya uongozi nikiwa bado kijana"Hivyo basi nanyie mnayonafasi ya kuhakikisha mnakuwa watu wema katika jamii yetu,mfano wa kuigwa,na hasa nategemea mafunzo haya yamewapa somo kubwa sana na mmeelimika vya kutosha namna ya kuwakiongozi na mtendaji mzuri kuanzia ngazi ya familia,Shina,tawi n.k kwa CCM.

 Mh.Mwigulu Nchemba akimtunuku mmoja wa vijana wa CCM, kuthibitisha kuwa amehudhuria mafunzo ya utendaji na uongozi wa umoja wa vijana.
Umoja wa vijana ndio siraha ya chama,mnategemwa sana kuzalisha viongozi wajao kutoka kwenye kundi hili.Nimeshawaona warithi wa Komba hapa(uimbaji),warithi wa Jenista Mhagama(uongozi) akina Dr,Emmanuel Nchimbi wapo hapa na hata Mh.Vita kawawa wingine yupo hapa.
Hivyo basi mnakila sababu ya kuendelea kuitetea CCM na kuhakikisha mnalinda heshima yake kwa nchi na nje ya nchi.hatupendi CCM kuwa kama vyama vingine ambavyo wezi wastaafu,wazinzi,mwenyekiti wake anapigana ngumi na mwenyekiti mwenzake hao wote kwao wanajiita makamanda na majembe.
 
 Mh.Mwigulu nchemba akisalimiana na kuzungumza machache na moja ya Mzee wa CCM anayeishi wilaya ya Namtumbo-Ruvuma.

CCM tunahitaji kuona makamanda wakweli na majembe ya kweli kama akina Nape Moses Nnauye,Sixtus mapunda na vijana wote wa UVCCM na viongozi wake wakizaliwa kutoka miongoni mwenu vijana wa Ruvuma.
Ni rai yangu kwako kijana wa CCM na wakitanzania  kuwa baada ya mafunzo haya kila mmoja wenu atakwenda kuwa mwalimu kwa mwenzake huko muendako.CCM ipo pamoja nanyi na hatuwezi kuipoteza benki hii ya vijana na tunaanza miradi mbalimbali ya chama kupitia kwenu.
 
 Mbunge wa Namtumbo Vita kawawa akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Mwigulu nchemba
Naye,Mbunge wa Namtumbo Mh.Vita Kawawa aliyekuwa mwenyeji wa   Mh.Naibu katibu mkuu alizungumza na vijana waliomaliza mafunzo yao kwa kuwambia "Wote mliopo hapa mmeona maendeleo yanayofanyika huku Ruvuma na hasa hapa Namtumbo,Mwaka 2010 hatukuwa na rami wala umeme,Leo tuna rami na umeme hapa.Naomba uchaguzi ujao muwe vinara wa kuifanya CCM iendelee kuongoza jimbo hili na dola ya nchi yetu.Vijana wenzangu huu ni muda wa kupambana sana na wapinzani wetu,hawana sera zaidi ya kusuka mipango ya kuharibu amani ya nchi na kufanya nchi isitawalike.Ilani ya CCM imetekelezwa ipasavyo na mnahaki ya kusimama na kuitetea CCM popote pale.Nipo tayari kuwasaidia kufanya mipango endelevu ya kujenga chama pamoja nanyi vijana wenzangu". 
Mbali na kuwa mgeni rasmi kwenye kufunga mafunzo ya vijana wa CCM hapa Namtumbo,Naibu katibu mkuu alipata nafasi ya kutembelea ujenzi wa ofisi za chama cha mapinduzi wilaya ya Namtumbo,ofisi kubwa wenye kujuisha jumuia zote za chama,car wash,Ukumbi wa mikutano na maeneo ya biashara(miradi ya chama).
 Mh.Mwigulu Nchemba akiingia kwenye ofisi za CCM wilaya ya Namtumbo,ofisi mpya ambazo bado zinaendelea kujengwa.Kushoto ni katibu wa CCM wilaya ya Namtumbo.
Mwigulu alitumia fursa hiyo kuwapongeza sana viongozi wa chama kuanzia ngazi ya mkoa,wilaya na had ngazi ya chini kabisa kwa namna wanavyoendelea kuijenga CCM na kuiimarisha ndani ya mkoa wa Ruvuma.
Wilaya ya Namtumbo ni mpya ikiwa na miaka saba(7) sasa tangu ianzishwe na Mbunge wake ni Vita Kawawa ambaye alikuwa mwenyeji wa Mh.Mwigulu Nchemba siku ya leo.CCM inashikilia kata zote za wilaya ya Namtumbo na inashikiliza vijiji vyote (serikali za mitaa).Hivyo CCM ndicho chama pekee kinachoongoza wilaya nzima ya Namtumbo.
 
 Naibu katibu mkuu akipewa maelekezo kutoka kwa katibu wilaya ya Namtubo wa CCM kuhusu maendeleo ya ujenzi wa ofisi za kisasa za chama.
 
 Naibu katibu mkuu akisaini kitabu cha wageni ofisi za CCM Namtumbo
 Mapenzi kwa chama kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto.Mh.Mwigulu alimzawadia hicho alichokishika mtoto mkononi.
Pia alipata wasaha wa kukutana na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh.Said Thabit Mwambungu ambapo walizungumzia hali ya maendeleo ya wilaya na hali ya kisiasa ndani ya mkoa wa Ruvuma.
 Naibu katibu Mkuu Tanzania bara -CCM akibadilishana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma
 Naibu katibu Mkuu alipomtembelea Dc wa wilaya ya Namtumbo ofisini kwake kabla ya kuelekea kwenye ufungaji wa mafunzo ya vijana wa CCM.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa