Home » » Kigogo wa UVCCM akanusha kuhusika na January Makamba

Kigogo wa UVCCM akanusha kuhusika na January Makamba


Naibu Waziri wa Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia, January Makamba
Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kupitia Mkoa wa Ruvuma, Halfan Kigwenembe, amesema kuwa hakuhusika kwa namna yoyote na mapokezi ya Naibu Waziri wa Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia, January Makamba, mjini Songea.
Makamba alikwenda mjini Songea, mkoani Ruvuma katikati ya mwezi huu na kukutana na baadhi ya wafanyabiashara ambao inadaiwa aliwaomba wamuunge mkono katika nia yake ya kugombea urais mwaka 2015.

Katika toleo la gazeti hili Novemba 18, mwaka huu tulichapisha habari iliyokuwa na kicha cha habari “January Makamba atinga Songea kusaka urais” huku Kigwenembe akitajwa kuwa alihusika kuwakaribisha wafanyabiashara hao kwenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kukutana na Makamba.

Akitoa ufafanuzi kwa gazeti hili kuhusiana na ziara ya Makamba, Kigwenembe alisema kuwa hakushiriki kwa namna yoyote katika ziara ya Makamba, ikiwamo kuwapokea wafanyabiashara katika ukumbi wa mikutano.

Kada huyo alisema kuwa wakati huo alikuwa nje ya Songea kwa shughuli zake za biashara.

 “Nilikuwa Dar es Salaam, tiketi za hoteli na ndege ninazo, kwa hiyo ieleweke kwamba sikushiriki kwa namna yoyote katika shughuli hiyo,” alisema Kigwenembe.
CHANZO: NIPASHE



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa