Home » » KINANA AFANYA MKUTANO WA HADHARA NA WANANCHI WA NAKAPANYA WILAYANI TUNDURU MKOANI RUVUMA,AWAHIDI KUMALIZA TATIZO LA BEI YA KOROSHO.

KINANA AFANYA MKUTANO WA HADHARA NA WANANCHI WA NAKAPANYA WILAYANI TUNDURU MKOANI RUVUMA,AWAHIDI KUMALIZA TATIZO LA BEI YA KOROSHO.

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akitolea ufafanuzi wa kina kwa Wakazi wa kijiji cha Nakapanya Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma mapema leo jioni,kuhusiana na tatizo sugu la bei ya zao la Korosho kwa wakulima,ambao wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu,Kinana aliwahakikishia Wanachi hao kuwa tatizo hilo watalifanyia kazi ipasavyo na kufikia hatua ya kulimaliza kabisa. 

Aidha tatizo hilo ni kubwa kwa upande wa mikoa ya Kusini,ikiwemo Mtwara,Lindi na Ruvuma.Kinana alibainisha kuwa CCM kitahakikisha suala la hilo linashughulikiwa kwa umakini  mkubwa ikishirikiana na Serikali sambamba na sambamba na taasisi zinazohusika na zao hilo,ili kukomboa uchumi wa Wananchi wa eneo hilo hasa kwa kuhakikisha viwanda vya kubangua korosho vinajengwa na vile ambavyo vimebinafsishwa na havifanyi kazi kunaandaliwa utaratibu ambao utawafanya wawekezaji wengine kupewa ili vifanye kazi na kutatua tatizo la bei ndogo ya zao hilo inayolipwa na wanunuzi. 

Katika ziara hiyo hiyo Kinana ameongozana na Katibu wa NEC siasa,Itikadi na uenezi Ndugu Nape Nnauye na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dkt.AshaRose Migiro. 
 Baadhi ya Wakazi wa kijiji cha Nakapanya Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wakishangilia jambo mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana,kuzungumzia na kufafanua vyema kuhusiana na tatizo kubwa lililopo kwenye zao la Korosho,ambako kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi ikiwemo suala la bei ya ununuzi wa Korosho kuwa ndogo,malipo kutokulipwa kwa wakati kwa wakulima na mengineyo.
Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini ,Mh.Ramo Matalla Makani akielezea baadhi ya matatizo yanayoisumbua Wilaya hiyo kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana  (pichani kulia) mapema leo,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Nakapanya,Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.Kinana na ujumbe wake wataanza ziara yao rasmi leoo Wilayani humo mkoani Ruvuma kwa madhumuni ya kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa Ilani ya CCM,katika Mikoa ya Ruvuma na Mbeya.
Baadhi ya Wakazi wa kijiji cha Nakapanya Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma wakiwa wamekusanyika mapema jana wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana,alipokuwa akizungumza nao kuhusiana na ufumbuzi wa matatizo yao mbalimbali ikiwemo suala la huduma za afya,Barabara,Maji sambamba na tatizo sugu la zao la Korosho wilayani humo.
Michuzi blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa