Home » » WANAOTUMIA KADI ZA BIMA YA AFYA ZA WALIOKUFA KUCHUKULIWA HATUA

WANAOTUMIA KADI ZA BIMA YA AFYA ZA WALIOKUFA KUCHUKULIWA HATUA


Mfuko wa Bima ya Afya Mkoani Ruvuma umefanikiwa kukusanya  kiasi cha Shilingi 182,573,809.36 sawa asilima 79 lengo likiwa kukusanya shilingi 228,668.000 kwa mwaka 2012 -2013

Meneja wa Bima ya Afya Mkoa wa Ruvuma  Siliveri Mgonja amesema hayo katika Mkutano wa wadau wa mfuko wa Afya ulio jumuisha wilaya tano za mkoa wa Ruvuma .

Akiwakilisha tarifa ya mafanikio na changamoto zinzo ikabili bima ya afya amesema moja ya changamoto ni pale wanapo fariki na vitambulisho vyao kutumika na familia iliyo baki.

Amesma hatua za kisheria zita chukuliwa kwa wale wote watakao bainika wa kitumia kadi za marehemu pia ameiomba serekari kutotoa fedha za mirathi mpaka kadi za Marehemu zirudishwe.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Saidi Thabiti Mwambungu amewataka watumishi wa serekari kuwa mfano bora kwa kuongoza kupima afya zao ili wananchi waige mfano wao wakujua afya zao.

Mganga Mkuu wa Hosipitali ya Mkoa wa Ruvuma Benedick  Ngaiza amesema Mfuko wa Bima ya Afya  unatakiwa kwenda na wakati kiwango kinacho tumilka cha malipo hakilingani na huduma zinazo tolewa akitoa mfano amesma huduma ya mama mja mzito bima hulipa shilingi 10.000/= lakini huduma hiyo kwa uhalisia ni shilingi 80,000

Mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi amesema Bima ya Afya ni mkombozi kwa wanyonge gharama wanazo lipa kwa familia moja ni kiasi kidogo sana amehimiza wananchi kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya

Hata hivyo wadau wa bima ya Afya walilalamikia upatikanaji wa dawa katika vituo vya Afya Vijijini na Mjini ,Halimashauri za miji na vjijini vime kuwa vikilipa fedha ndogo kwa waheshimiwa madiwani badala ya kulipa asilimia 6 hulipa asilimia 3 tu na kuacha mzigo mkubwa kwa mfuko wa bima ya afya.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa