Home » » MTOTO WA MAIAKA 5 AJERUHIWA VIBAYA NA PANGA AKIMTHUMU KUIBA MAPERA HUKO SONGEA.

MTOTO WA MAIAKA 5 AJERUHIWA VIBAYA NA PANGA AKIMTHUMU KUIBA MAPERA HUKO SONGEA.


Mtoto Benson Tole akiwa na mama yake MTOTO Mmoja BENSON TOLE mwenye umri wa miaka Mitano mkaz...


Mtoto Benson Tole akiwa na mama yake
MTOTO Mmoja BENSON TOLE mwenye umri wa miaka Mitano mkazi wa Ruhuwiko mjini Songea mkoani Ruvuma, amenusurika kifo baada ya kukatwakatwa kwa kitu chenye ncha kali sehemu za usoni na Mzee mmoja LONGINUS HAULE mwenye miaka 51 akimtuhumu mtoto huyo kumuibia matunda aina ya Mapera shambani kwake. 

Mtoto BENSON TOLE kwa sasa amelazwa katika hospitali ya mkoa mjini Songea katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU), Madaktari wanaendelea kunusuru uhai wa mtoto huyu baada ya kupata mashambulio makali ya kucharangwacharangwa na kitu chenye ncha kali sehemu za usoni na mtuhumiwa mmoja LONGINUS HAULE mkazi wa Polisi Lizaboni mjini Songea. 

Mzee HAULE anatuhumiwa baada ya kumfanyia unyama wa kutosha mtoto huyo na kisha kupoteza fahamu akimtuhumu kumuibia matunda aina ya mapera shambani kwake alimtupia kwenye nyumba moja ambayo haijaisha ujenzi wake akidhani tayari ameshamuua. 
Afisa Muuguzi wa Hospitali ya mkoa mjini Songea, JOSEPH MTEWELE amesema kwa sasa mtoto huyo yupo chini ya uangalizi maalumu na kwamba madaktari wanaendelea na jitihada za kunusuru uhai wake kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata sehemu za kichwani. Jeshi la polisi mkoani Ruvuma limetihibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba linaendelea kuchukua hatua zaidi za kumfikisha Mzee LONGINUS HAULE kwenye vyombo vya sheria kwa hatua zaidi. 

Credit: Emmanuel Msigwa Channel Ten Songea.

CHANZO BLOG YA JESTINA GEORGE







0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa