Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani
amesema, serikali haitamvumilia na kumuonea huruma mkurugenzi wa
halmashauri, mji, manispaa na jiji ambaye atashindwa kasi ya utendaji wa
Serikali ya Awamu ya Tano.
Mbali na hilo, Naibu Waziri amewaagiza wakurugenzi wote hapa nchini
kutumia rasilimali za msitu zilizoko katika wilaya zao kumaliza tatizo
la madawati na kusema kwamba hakuna mwanafunzi yeyote atakayekaa chini
kwa kukosa dawati.
“Agizo hili ni la serikali ya awamu ya tano, sisi hatuangalii wapi ni
lazima uwajibike pale unapoona mambo hayaendi vizuri, hata mkurugenzi
wangu na wewe agizo hili linakuhusu, mkurugenzi tumia rasilimali...
WANAWAKE WAHAMASISHWA KULETA MAENDELEO.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WANAWAKE wilayani Songea, Ruvuma wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko
ya kiuchumi hapa nchini kwa kuwa mfano bora katika kufanya kazi za
kujiletea maendeleo.
Wameelezwa wakifanya hivyo, itawawezesha kubadili mawazo na mtazamo
kwamba mwanamke ni kiumbe dhaifu anayehitaji kusaidiwa kwa kila kitu
katika maisha yake.
Mbali na hayo, wameaswa kutumia uwezo wao kuibadili jamii ya
kitanzania kitabia na kifikra dhidi ya mtazamo kwamba mtoto wa kike
ndiye anayeongoza katika suala zima la mmomonyoko wa maadili,
unaosababishwa na kuingia kwa utandawazi.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na diwani wa Ndilimalitembo katika
Manispaa ya Songea, Cresensia Kapinga,...
Mbunge Kessy ataka serikali ibane matumizi zaidi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mbunge wa Nkasi kaskazini Ally
Keissy amewataka wabunge waungane kukataa matumizi ya serikali kuwaleta
wakurugenzi,wakuu wa mikoa pamoja madereva kwenda Dodoma kushiriki
vikao vya Bunge kwani fedha nyingi hupotea bila mafanikio kuonekana.
Kessy ameyasema hayo wakati akichangia mjadala wa kuijadili hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 11.
''Huu utaratibu wa kuwaleta
madereva, na wakurugenzi pamoja na wakuu wa mikoa ni lazima wabunge
tuungane kupinga matumizi yasiyo...
MWALIMU AKUTWA AMEJINYONGA CHUMBANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Revocatus Malimi.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Peramiho, Songea mkoani
Ruvuma, Baraka Mwakajila (29), amekutwa amefariki dunia baada ya
kujinyonga kwa kutumia shati ndani ya nyumba alimokuwa akiishi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Revocatus Malimi, alisema
jana kuwa tukio hilo limetokea juzi saa sita mchana katika mji mdogo wa
Peramiho, nje kidogo ya Manispaa ya Songea.
Malimi alisema inadaiwa kuwa siku hiyo...
ELIMU BURE BADO KIZUNGUMKUTI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Dk. John Magufuli.
Wakati utekelezaji wa mpango wa elimu bure ya Rais
Dk. John Magufuli, ukianza jana, baadhi ya wazazi wamekumbwa na
sintofahamu baada ya wanafunzi kurudishwa nyumbani wakidaiwa michango na
maeneo mengine utitiri wa wanafunzi ukiwa kikwazo, huku kwingine mwamko
wa uandikishaji ukiwa chini.
Mwishoni mwa mwaka jana, serikali ilitoa mwongozi wa elimu ya
msingi (shule ya msingi mpaka kidato cha nne) kuwa wazazi watatakiwa
kununua sare za shule na michezo, madaftari,...
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu ametembelea jengo la zahanati ya Mpingi, wilaya ya Songea Vijijini
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy
Mwalimu ametembelea jengo la zahanati ya Mpingi, wilaya ya Songea
Vijijini na kuzungumza na wanakijiji wa eneo hilo.
Ziara hiyo ni moja kati ya kazi anazozifanya mkoani hapa kwa lengo la
kuzungumza na wananchi, watoa huduma na watumishi wa sekta ya afya ili
kuboresha huduma za matibabu na kuhamasisha wananchi kushiriki katika
shughuli mbalimbali za afya ikiwemo uchangiaji katika mfuko wa Bima ya
Afya.
Baada ya kufika kijijini hapo...
Waziri Ummy Mwalimu atembelea jengo la zahanati ya Mpingi wilaya ya Songea

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Mwandishi Maalum
WAZIRI WA AFYA Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa
Ummy Mwalimu ametembelea jengo la zahanati ya Mpingi wilaya ya Songea
Vijijini na kuzungumza na wanakijiji wa eneo hilo.
Ziara hiyo ni moja kati ya kazi anazozifanya mkoani hapa kwa lengo la
kuzungumza na wananchi, watoa huduma na watumishi wa sekta ya afya ili
kuboresha huduma za matibabu na kuhamasisha wananchi kushiriki katika
shughuli mbalimbali za afya ikiwemo uchangiaji katika mifuko ya afya
...
Ziara ya Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa NHC Ruvuma
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Nyumba za gharama nafuu NHC Mkuzo Songea zinavyoonekana kwa sasa.
Meneja
wa Shirika la Nyumba mkoa wa Ruvuma, Saidi Bungara akiongozana na
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo, Pius Tibazarwa alipokuwa kwenye ziara ya
mradi wa nyumba za gharama nafuu Mkuzo, Songea.
Meneja wa Shirika la Nyumba mkoa wa Ruvuma, Saidi Bungara akimwelekeza
jambo Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo, Pius Tibazarwa alipokuwa kwenye
ziara ya mradi wa nyumba za gharama nafuu Mkuzo, Songea.
Meneja
wa Shirika la Nyumba mkoa wa...
MAJALIWA: NAFARIJIKA KUONA WAZEE WANAPATA MATIBABU BURE TENA BILA USUMBUFU
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa amefarijika kuona wazee wanapata huduma za matibabu bure na kwa utaratibu mzuri katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.
Akizungumza na madaktari, wauguzi na watumishi wengine wa hospitali hiyo wiki hii, alivyokuwa kwenye ziara mkoani humo, Waziri Mkuu Majaliwa amesema utaratibu wa kutenga chumba maalum chenye madaktari wawili mahsusi kwa ajili ya kuwahudumia wazee unaotekelezwa hospitalini hapo umeondoa adha kubwa kwa wazee kusubiri...
WAZIRI MKUU ATEMBELEA KIWANDA CHA TUMBAKU MKOANI RUVUMA NA KUWASIMAMISHA KAZI VIONGOZI WA CHAMA CHA USHIRIKA CHA SONAMCU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha kusindika tumbaku cha
mkoani Ruvuma na kuwasimamisha kazi viongozi wa Chama Cha Kikuu Cha
Ushirika cha SONAMCU.
Akizungumza
jana jioni(Jumanne, Januari 5, 2016), katika ukumbi wa mikutano wa
Ikulu Ndogo ya Songea, wakati alipokutana na wakulima wa zao la tumbaku
wa Wilaya ya Namtumbo, Wananchama wa Vyama Vya Ushirika vya Mkoa wa
Ruvuma, viongozi wa Mkoa pamoja na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Edwin Ngonyani ambaye ni Mbunge...
WAZIRI MKUU,KASSIM MAJLIWA ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA RUVUMA.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
Mkuu,Kassim Majliwa akizungumza na baadhi ya wananchi waliofika
kuwahudumia wagonjwa wao waliolazwa kwenye hospitali ya mkoa wa Ruvuma
baada ya kuitembelea akiwa katika ziara ya mkoa huo Januari 5,
2016.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo, Thabiti Mwabungu na kulia ni Mbunge wa
Songea Mjini, Leonidas Gama. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Thabiti
Mwambungu.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa,akimsalimia mtoto Flora Mapunda (1) ambaye
amelazwa katika hospitali ya Mkoa...
WAZIRI MKUU AKAGUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa amekagua jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya
Wialaya ya Songea lilipo katika kijiji cha Lundusi, Wilaya ya Peramiho
mkoani Ruvuma.
Alipowasili
jana katika eneo hilo alikutana na viongozi wa jadi ambapo Mzee
Daniel Gama alimkabidhi ngao na silaha ikiwa ni ishara ya kumkaribisha
kijijini hapo, pia alipata fursa ya kutazama ngoma ya mila ya kabila la
Wangoni.
Mara
baada ya kukagua jengo hilo la ghorofa,Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Lundusi Bwana...
WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA NFRA NA UJENZI WA OFISI YA MKURUGEZI PERAMIHO
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
Mkuu, Kassim Majliwa akikagua mahindi yaliyohifadhiwa nje ya majengo ya
maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA mjini Songea
akiwa katika ziara ya siku tatu mkoani Ruvuma Januari 4, 2016. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majliwa akikagua mahindi yaliyohifadhiwa nje ya majengo ya
maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA mjini Songea
akiwa katika ziara ya siku tatu mkoani Ruvuma Januari 4, 2016. (Picha na
Ofisi...