Home » » Mbunge Kessy ataka serikali ibane matumizi zaidi

Mbunge Kessy ataka serikali ibane matumizi zaidi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Mbunge wa Nkasi kaskazini Ally Keissy amewataka wabunge waungane kukataa matumizi ya serikali kuwaleta wakurugenzi,wakuu wa mikoa pamoja madereva kwenda Dodoma kushiriki vikao vya Bunge kwani fedha nyingi hupotea bila mafanikio kuonekana.

Kessy ameyasema hayo wakati akichangia mjadala wa kuijadili hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 11.

''Huu utaratibu wa kuwaleta madereva, na wakurugenzi pamoja na wakuu wa mikoa ni lazima wabunge tuungane kupinga matumizi yasiyo ya lazima,hapa na tuanze na hawa maana kuwasafirisha wakuu wote hawa nchi nzima kuja Dodoma hizo fedha zingeelekezwa katika sehemu nyingine kusaidia miradi ya wananchi''Amesisitiza Kessy.

Aidha Kessy ameiomba serikali kumuunga mkono jimboni kwake katika kwenda kuhakiki fedha zilizotumwa kwa ajili ya miradi ya maji na mbolea kwa wakulima kwani fedha nyingi zimeliwa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa