Home » » ASIYEKWENDA NA KASI YA SERIKALI KUTOVUMILIWA.

ASIYEKWENDA NA KASI YA SERIKALI KUTOVUMILIWA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani amesema, serikali haitamvumilia na kumuonea huruma mkurugenzi wa halmashauri, mji, manispaa na jiji ambaye atashindwa kasi ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Mbali na hilo, Naibu Waziri amewaagiza wakurugenzi wote hapa nchini kutumia rasilimali za msitu zilizoko katika wilaya zao kumaliza tatizo la madawati na kusema kwamba hakuna mwanafunzi yeyote atakayekaa chini kwa kukosa dawati.
“Agizo hili ni la serikali ya awamu ya tano, sisi hatuangalii wapi ni lazima uwajibike pale unapoona mambo hayaendi vizuri, hata mkurugenzi wangu na wewe agizo hili linakuhusu, mkurugenzi tumia rasilimali za miti zilizoko katika halmshauri yako kupunguza tatizo la madawati kama lipo,” alisema Ngonyani.
Naibu Waziri ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na madiwani na baadhi ya watumishi wa halmashauri ya Namtumbo katika kikao cha Baraza la Madiwani.
Alisema amepiga marufuku tabia ya madiwani kufanya biashara na halmashauri kwa kuwa jambo hilo linaweza kuleta mtafaruku kwa halmashauri na hivyo kushindwa kukamilika kwa miradi ya maendeleo.
Alisema hata yeye japokuwa ni mbunge wa jimbo hilo, hatoweza kufanya biashara Na halmashauri kwani ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma hivyo kila kiongozi kuanza kujitafakari nafasi aliyonayo kwa wananchi.
Aidha amewataka madiwani hao kuhakikisha kwamba wanashirikiana na watumishi wa halmashauri kupunguza tatizo la uhaba wa matundu ya choo, madawati na upungufu wa zahanati katika maeneo yao.
CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa