Home » » Waziri Ummy Mwalimu atembelea jengo la zahanati ya Mpingi wilaya ya Songea

Waziri Ummy Mwalimu atembelea jengo la zahanati ya Mpingi wilaya ya Songea

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

images 
Na Mwandishi Maalum
 WAZIRI WA AFYA Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu ametembelea jengo la zahanati ya Mpingi wilaya ya Songea Vijijini na kuzungumza na wanakijiji wa eneo hilo. Ziara hiyo ni moja kati ya kazi anazozifanya mkoani hapa kwa lengo la kuzungumza na wananchi, watoa huduma na watumishi wa sekta ya afya ili  

kuboresha huduma za matibabu na kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli mbalimbali za afya ikiwemo uchangiaji katika mifuko ya afya Baada ya kufika kijijini hapo na kuona jitihada zilizofanywa na Halmashauri na wananchi, Waziri Ummy aliwaahidi wananchi hao mabati na misumari ili kuunga mkono ujenzi wa zahanati hiyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa