Home » » WANAWAKE WAHAMASISHWA KULETA MAENDELEO.

WANAWAKE WAHAMASISHWA KULETA MAENDELEO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WANAWAKE wilayani Songea, Ruvuma wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kiuchumi hapa nchini kwa kuwa mfano bora katika kufanya kazi za kujiletea maendeleo.
Wameelezwa wakifanya hivyo, itawawezesha kubadili mawazo na mtazamo kwamba mwanamke ni kiumbe dhaifu anayehitaji kusaidiwa kwa kila kitu katika maisha yake.
Mbali na hayo, wameaswa kutumia uwezo wao kuibadili jamii ya kitanzania kitabia na kifikra dhidi ya mtazamo kwamba mtoto wa kike ndiye anayeongoza katika suala zima la mmomonyoko wa maadili, unaosababishwa na kuingia kwa utandawazi.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na diwani wa Ndilimalitembo katika Manispaa ya Songea, Cresensia Kapinga, wakati akizungumza na wanawake wajasiriamali wa kata hiyo wanaojishughulisha na biashara ndogo ikiwemo matunda na mboga.
Alisema hivi sasa kuna vitendo vya mmomonyoko mkubwa wa maadili hapa nchini ambapo vijana wanaiga mienendo ya kigeni na wakati na kuacha mila na desturi ya Mtanzania, jambo ambalo ni hatari.
Kwa mujibu wa Kapinga ni kwamba vitendo hivyo vinahitaji nguvu ya pamoja kwa wazazi na walezi na hata kwa jamii husika kwa sababu tayari imeonekana katika baadhi ya familia mzazi anashindwa kukemea tabia hizo na kusababisha vijana wengi kuangamia.
Alisema asilimia kubwa ya watoto wa kike wanaambukizwa virusi vya Ukimwi na vijana wa kiume wanaingia katika matumizi zaidi ya dawa za kulevya.
CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa