Home » » MADAKTARI WATAKIWA KUPUNGUZA SAFARI NA SEMINA

MADAKTARI WATAKIWA KUPUNGUZA SAFARI NA SEMINA

Mwandishi wetu, Ruvuma Yetu
 
Madaktari Mkoani Ruvuma wametakiwa kutojilimbikizia Madaraka kwa kujipangia kila Semina na mikutano kuhudhulia wao huku wenzao wakiganga njaa, huo sio Utawala bora.
                    
Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma ameyasema hayo wakati akifungua Semina ya siku 2 ya kutathmini mafanikio na Changamoto zinazoikabili Sekta ya Afya Mkoani Ruvuma.
 
Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Hasani Bendeyeko amesema shughuli nyingi ambazo zinatakiwa kufanywa na Madaktari mara zote hukwama kutokana na Madaktari kuwa safarini kuhudhuria semina.

Alisema wakati mwingine daktari mmoja anweza kuhudhuria semina zaidi ya Saba mfululizo na kuacha shughuli za utendaji zikidorora katika hospitali.

Katibu tawala mkoa wa Ruvuma amesema kubadilishana safari nako kunaleta uzoefu kwa anayeenda semina.
 
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa