Home » » MBUNGE WA PERAMIHO ATOA MSAADA WA PIKIPIKI

MBUNGE WA PERAMIHO ATOA MSAADA WA PIKIPIKI

Na Amon Mtega, Songea
MBUNGE wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama, ameto msaada wa pikipiki saba zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 10 kwa makatibu kata wa chama hicho wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Msaada huo aliutoa jana katika Kijiji cha Lipokela kilichopo Kata ya Mbingamhalule kwa nia ya kuwarahisishia utendaji kazi wao ndani ya chama kwa ajili ya kuendana na mfumo wa siasa za sasa.

Kata zilizonufaika na msaada huo wa pikipiki ni Kikunja, Mtyangimbole, Muungano, Mpandangindo, Mkongotema na Mbingamhalule.

Akikabidhi msaada huo, aliwataka makatibu kata hao kutambua kwamba pikipiki hizo walizokabidhiwa si mali yao binafsi bali zitatumika kwa ajili ya shughuli zote za chama na Serikali, ikiwamo kusaidia kubebea wagonjwa katika maeneo yao.

Aidha, alitoa msaada wa trekta dogo za kulimia lenye thamani ya Sh milioni tisa kwa wananchi wa Kijiji cha Lipokela kama ahadi yake aliyoitoa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyoifanya mapema mwaka huu mkoani Ruvuma.

Naye, Diwani wa Kata ya Mbingamhalule, Nasri Nyoni, alimshukuru na kumpongeza mbunge huyo kwa michango yake anayoitoa kwa wananchi, kwa ajili ya kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya jimbo hilo.
Chanzo: Mtanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa