Home » » TTCL YALALAMIKIA WIZI WA NYAYA ZA SIMU

TTCL YALALAMIKIA WIZI WA NYAYA ZA SIMU

Na Amon Mtega, Songea
MENEJA wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) mkoani Ruvuma, Dadiely Chanachayo, amelalamikia vitendo vya wizi wa nyaya za simu. Malalamiko hayo alitoa mjini hapa jana kutokana na wizi uliojitokeza kwa baadhi ya wananchi kuiba nyaya za simu na kusababishia baadhi ya wananchi kukosa huduma ya mawasiliano.

Alisema wizi huo umesababisha baadhi ya taasisi kushindwa kutoa huduma muhimu kwa wananchi wake ikiwamo Benki ya NMB.

Alisema watu hao wanaiba nyaya hizo kwa ajili ya kutafuta waya wa ndani uitwayo kopa kwa lengo la kutengenezea bidhaa mbalimbali ikiwamo mapambo ya kuvaa mikononi ikiwamo bangili.

Aidha, alisema katika kukabiliana na tatizo hilo wamejiwekea utaratibu wa kutoa zawadi kwa wale watakaotoa taarifa ya watu wanaofanya vitendo hivyo.

Aliwataka wananchi kuacha tabia ya kuharibu miundombinu ya mawasiliano kwa kuwa kufanya hivyo ni kuisababishia Serikali hasara ambazo hazikustahili.
Chanzo: Mtanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa