Home » » ‘DOSARI ZA SENSA ZINATOKANA NA AHADI HEWA ZA SERIKALI’

‘DOSARI ZA SENSA ZINATOKANA NA AHADI HEWA ZA SERIKALI’


Mwandishi wetu, Songea-Ruvuma Yetu
 
Wananchi walioshiriki zoezi la Sensa Mkoani Ruvuma wameiomba Serikali kuacha kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki kwa kuwa ni moja ya mambo yanayopunguza imani ya wananchi kwa serikali yao hasa katika mambo muhimu kama sense.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati wa Zoezi la Sensa la kuhesabu watu ambalo linaendelea kufanyika Mkoani Ruvuma wamesema ahadi nyingi zisizotekelezeka ndiyo kero kubwa kwa wananchi.
 
Maruzuku Mohamed Mkaazi wa Manspaa ya Songea amesema ili Serikali iweze kufanya kazi vizuri inapaswa kuwa na Kamati ya kufuatilia ahadi zinazotolewa na Viongozi ili kupunguza tabia ya viongozi kutoa ahadi hewa kila mara.

“Ahadi zimekuwa nyingi kiasi hata wananchi wanashangaa kuona kila kiongozi akitoa ahadi ya kuleta kitu Fulani halafu hawatekelezi ni vizuri kuunda kamati ya kufutilia ahadi za viongozi”
 
 
Vijana walioshiriki Sensa ya watu na Makazi wamesema Serikali ijitahidi kuwapatia ajira Vijana ndipo atakapoona umuhimu wa Sensa.

Vijana wamesema toka tupate uhuru kasi ya ongezeko la watu ni kubwa kutoka watu milioni 9 kabla ya uhuru hadi kufikia watu milioni 40 lakini pamoja na kasi hiyo walio wengi ni vijana na kwamba sensa ni lazima iwajali vijana hao.
 
Blogszamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Ruvuma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa